Kenya: Wanawake walinzi wapambana na ujangili na chuki
Katikati ya Kenya, kundi la wanawake wa Kimasai wanavunja imani potofu za jamii yao. Timu ya Lioness, wanawake wote wa askari wa doria, wanatano ulinzi wa wanyamapori wa nyanda za kusini mwa nchi. Dhamira yao: kulinda wanyamapori na kupambana na ubaguzi katika jamii ya mfumo dume.
Imechapishwa:
Katikati ya Kenya, chini ya jua kali, walinzi wa kike wa Team Lioness wamekuwa wakipiga doria katika nyanda za kusini mwa Kenya. Kundi hili la wanawake wa Kimasai linavunja dhana potofu za jamii yao.
Team Lioness, wanawake wote wa askari wa doria, wanatoa ulinzi wa wanyamapori wa nyanda za kusini mwa nchi. Wanawake hawa jasiri wanappambana sio tu dhidi ya ujangili, lakini pia dhidi ya chuki iliyoota mizizi katika jamii ya mfumo dume.
Wakiwa wamefunzwa na kupewa vifaa na IFAW, wanawake hawa wa Kimasai wanakabiliana na majangili na mila za mababu. "Jumuiya yangu haikufikiria kuwa mwanamke angeweza kustahimili kazi hii," anasema Purity Lakara, kiongozi wa kundi hili.
Kuwa mlinzi ilikuwa ndoto kwa Sharon Nankinyi. Familia yake hapo awali ilipinga, ikimhukumu kuwa hawezi kutimiza kazi kama hiyo. Lakini uvumilivu wake hatimaye ulizaa matunda. “Tuliandamana tukiwa tumevalia sare, tulishirikiana na watu, na kuonyesha uwezo wetu,” amesema kwa fahari.
Ujasiri wao na kujitolea kwao viliwashawishi wakazi hatua kwa hatua.“Wanatutia moyo,” anakiri Naiswaku Parsitau, kiongozi wa Wamasai. "Hata usiku, wanaitikia wito weto na kulinda mifugo yetu."
Team Lioness iliyoundwa mwaka wa 2019, ni ishara ya matumaini kwa wanawake wa Kimasai. "Wanathibitisha kuwa wanawake wanaweza kufaulu katika nyanja zote," anasema Kenneth Saei, kiongozi wa jumuiya.
Huko katika kijiji chake cha asili, Sharon Mumbi, 21, ni chanzo cha motisha kwa wasichana wadogo. "Mimi ndiye mlinzi pekee wa kike katika eneo hili, na ninataka kuwaonyesha wengine kwamba chochote kinawezekana," anasema kwa ujasiri.
Pambano la walinzi wa kike wa Team Lioness liko mbali sana, lakini ujasiri na dhamira yao inawafanya waanzilishi wa mabadiliko katika jamii yao.