Mpishi wa Nigeria athibitishwa na Guinness Book of World Records
NAIROBI – Mpishi wa Nigeria ambaye amekuwa maarufu nchini humo baada ya kupika bila kukoma kwa zaidi ya saa tisini na tatu amethibitishwa kuwa mshikilizi mpya wa rekodi ya dunia.
Imechapishwa:
Wanasiasa na watu mashuhuri walimshangilia Hilda Baci wakati akiwa jikoni kwake huko mjini Lagos wakati alipopika kwa kipindi cha siku nne mwezi uliopita.
Alitumia zaidi ya sahani 100 katika mchakato huo na aliruhusiwa tu kuchukua mapumziko ya dakika tano kila saa.
— Guinness World Records (@GWR) June 13, 2023
Baci amemshinda mshikilizi wa zamani wa rekodi ya dunia Lata Tondon wa India, ambaye alikuwa anashikilia rekodi hiyo kwa muda wa saa 87 dakika 45 mwaka wa 2019.
The Guinness Book of World Records, ambao walichunguza tukio hilo la kupikika, wamempongeza kwa kupitia ujumbe wa video:
After reviewing all the footage, we're delighted to announce that Hilda Baci is the new record holder for the longest cooking marathon (individual) 💫
— Guinness World Records (@GWR) June 13, 2023
Watch the video to find out the official time we've awarded Hilda and read the full explanation below 👇 pic.twitter.com/bf352ndxWO