WHO yataka kuepo na makubaliano ya kupambana na magonjwa ya milipuko
Shirika la Afya Duniani, WHO, linakutana katika kikao maalum kuunda mkataba juu ya milipuko wa Covid-19. WHO pia imepinga vikwazo vinavyoathiri kusini mwa Afrika baada ya ugunduzi wake juu ya aina mpya ya kirusi cha Omicron.
Imechapishwa:
Hii ni mara ya pili katika historia yake kwa WHO kukutana katika kikao maalum, ameeleza mwanahabari wetu mjini Geneva, Jérémy Lanche. Hii inakuja katikati ya mlipuko wa maambukizi ya virusi vya Corona huko Ulaya, na siku chache tu baada ya wanasayansi wa Afrika Kusini kugundua uwepo wa aina mpya ya kirusi cha Omicron.
Wakati Mataifa mengi zaidi yanajizuia katika kukabiliana na tishio hili jipya, WHO inatoa wito badala yake kuacha mipaka wazi, hasa na Afrika Kusini. Kwa upande wa shirika la Afya Duniani, hatua hizi hazina tija.
Muchas gracias #Chile Health Minister @DrEnriqueParis for your leadership on a #PandemicTreaty/accord at the #WHASpecial. We welcome your support, including for strengthening and sustainable financing of @WHO. We also discussed 🇨🇱's effective management of the #COVID19 response pic.twitter.com/0SGpdrqUTl
— Tedros Adhanom Ghebreyesus (@DrTedros) November 29, 2021
Ikiwa nchi itatangaza kuibuka kwa aina mpya ya kirusi kwenye ardhi yake, na kwamba kwa kujibu haua za kuitenga zinachukuliwa, basi ni kusubiri hatari katika siku zijazo, nchi hazitashirikiana kwa uwazi. Aidha, vikwazo hivi havijazuia tofauti ya B1.1.529 kuenea, kwa kuwa tayari imetambuliwa katika mabara kadhaa ya dunia.
Kutokana na tishio hili ambalo bado linaweza kupimwa kwa usahihi si maambukizi au ugonjwa, kwa kukosa mtazamo, WHO inasihi kuchunguzwa upya kwa mikataba ya kimataifa inayoelekea ushirikiano zaidi. Hii ndiyo maana halisi ya kikao.
Kwanza, kuna suala la upatikanaji wa chanjo: ikiwa hakuna usawa katika kugawana chanjo, na nchi zilizohifadhiwa kwa upande mmoja na nchi mbazo inasema virusi vinazunguka kwa upande mwingine, hii kwanza inaleta tatizo la kimaadili, na hii ni kuchukua hatari ya kuona aina mpya ya kirusi inaibuka. WHO imekuwa ikionya kuhusu hili kwa miezi kadhaa. Omicron inaonyesha kwamba matokeo yalikuwa sahihi, anabainisha Simon Rozé, anayesimamia maswali ya kisayansi katika RFI.
This is a historic moment for countries to agree on a common, binding approach to a common threat coming from our relationship with nature. It won't solve every problem, but it will provide the framework to foster greater cooperation & strengthening 🌍 health security #WHASpecial pic.twitter.com/YjatVOE5lo
— Tedros Adhanom Ghebreyesus (@DrTedros) November 29, 2021