DRC/Rwanda : Yakubaliana kumaliza tofauti zao
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda, zimekubaliana kuanza mchakato wa kumaliza tofauati zao, baada ya mkutano wa marais wa nchi hizo mbili waliokutana jana jijini Luanda nchini Angola.
Imechapishwa:
Msuluhishi wa mvutano wa wiki kadhaa kati ya nchi hizo jirani, rais wa Angola Joao Lourenco, ametangaza kuwa pande mbili zimekubaliana kusitisha mvutano kati, bila ya kueleza kwa undani wa kilichoafikiwa.
Hata hivyo, Ofisi ya rais Felix Thisekedi, kupitia msemaji wake Erick Nyindu amesema watahakikisha makubaliano yalioafikiwa yanatekelezwa kwa lengo la kupata amani Mashariki mwa DRC na kwamba kuna matumaini uhusiano kati ya Rwanda na DRC utaimarika tena, Nyindu akiongeza kuwa DRC, itahakikisha wakimbizi hasa wa FDLR na wengine wanarudi wanarejeshwa Rwanda.
Aidha, ripoti zinaeleza kuwa mkutano huo ulikuja na mambo sita ambayo nchi hizo zinataka yatekelezwa ikiwemo kurejesha uhusiano wa kidiplomasia lakini pia kuacha kutumia makundi ya waasi ya M 23 na FDLR kutishia usalama wa nchi hizo mbili.
Kamati ya pamoja kati ya DRC na Rwanda itaundwa kuhakikisha uteketelezwaji wa mambo yaliyokubaliwa na inatarajiwa kukutana jijini Luanda tarehe 12 mwezi huu.