TB bado inasababisha vifo vya wengi Afrika Mashariki
Dunia inaadhimisha siku ya TB kila Machi 24 huku kukiwa na wito wa kupunguza vifo vinavyohusishwa na TB na kuimarisha matibabu ya TB
Imechapishwa:
Cheza - 00:43
Wakati dunia inapoadhimisha siku ya kupiga vita maambukizi ya Kifua Kikuu au TB, ugonjwa huo unaoenekana kuendelea kuwa hatari na kusababisha idadi kubwa ya vifo katika nchi za Afrika Mashariki, licha ya kuwepo kwa dawa kwa miaka 60 sasa.
Ripoti ya shirika la United for Global Mental Health,idadi ya watu walio na TB wanaopata matatizo ya akili ,huenda ikafikia asilimia 50 kufikia mwaka 2030 iwapo serikali za dunia hazitaonisha swala la afya ya akili kwenye mapambano ya kumaliza TB.
Lucy Wanjiku Maina ni mwazilishi wa shirika la kiraia la Positive Young Women Voices jijini Nairobi .