Pata taarifa kuu

DR Congo yakanusha kuingia makubaliano ya kijeshi na Urusi

Nairobi – Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imekanusha ripoti kwamba imetia saini mkataba wa ushirikiano wa kijeshi na Urusi.

Wanajeshi wa FARDC wakipiga doria mashariki ya DRC, Tarehe 15 Novemba 2022.
Wanajeshi wa FARDC wakipiga doria mashariki ya DRC, Tarehe 15 Novemba 2022. REUTERS - ARLETTE BASHIZI
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa ya wizara ya mawasiliano na vyombo vya habari nchini DR Congo siku ya Alhamisi, hakuna makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi yaliyotiwa saini hivi karibuni kati ya Urusi na Kinshasa .

Taarifa hiyo ya serikali imekuja baada ya ile iliyochapishwa na shirika la habari la serikali ya Urusi TASS siku ya Jumanne, ambayo ilisema kuwa serikali ya Urusi iliidhinisha rasimu ya makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi na DR Congo.

Kwa mujibu wa TASS makubaliano hayo yalihusisha mazoezi ya pamoja, mafunzo ya kijeshi na masuala mengine ya kiusalama.

Shirika la habari la Urusi wiki hii lilithibitisha kuwepo kwa makubaliano hayo kati ya Moscow na Kinshasa

DR Congo inasema rasimu ya makubaliano husika ilianzishwa na nchi hizo mbili mwaka 1999, lakini bado haijatiwa saini.

Urusi imekuwa ikikuza mikataba yake ya kijeshi na nchi za Kiafrika huku ikijaribu kupanua ushawishi wake wa kisiasa katika bara hilo.

Kupitia kundi la mamluki la Wagner, Urusi imekuwa ikitoa msaada wa kijeshi kwa Jamhuri ya Afrika ya Kati na serikali zinazoongozwa na serikali za Mali, Niger na Burkina Faso.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.