Pata taarifa kuu

DRC: Mapigano yaripotiwa kati ya FARDC na M23 Kilolirwe na Kitshanga

Nairobi – Mapigano yalizuka tena hapo jana kati ya jeshi la Serikali ya DRC, FARDC na M23 kwenye maeneo ya Kilolirwe na Kitshanga, wilayani masisi jimboni Kivu Kaskazini, baada ya siku chache za kusitisha mapigano.

Wanajeshi wa DRC wamendelea kupambana na makundi ya watu wenye silaha mashariki ya taifa hilo
Wanajeshi wa DRC wamendelea kupambana na makundi ya watu wenye silaha mashariki ya taifa hilo AFP - SEBASTIEN KITSA MUSAYI
Matangazo ya kibiashara

Hali imeripotiwa kuwa ya wasiwasi katika mji wa Kishanga, ambako vyanzo kadhaa vimedai kuwa wanajeshi wa Burundi waliondoka kwenye eneo hilo baada ya kambi yake kushambuliwa, taarifa ambazo hata hivyo bado hazijathibitishwa na jeshi la kikanda la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wanajeshi wa Afrika Mashariki na wale ya serikali ya DRC wamekuwa wakipambana na makundi ya waasi
Wanajeshi wa Afrika Mashariki na wale ya serikali ya DRC wamekuwa wakipambana na makundi ya waasi AFP - ALEXIS HUGUET

Aidha hali ya utulivu iliripotiwa kwenye mji wa Rutshuru, baada ya mapigano makali yaliyohusisha silaha nzito siku ya Jumanne.

Mashirika ya kiraia kwenye maeneo hayo, yameripoti vifo vya watu na wengine mamia kujeruhiwa, ingawa mamlaka hazijatoa takwimu rasmi kuhusu watu waliopoteza maisha katika mapigano hayo.

Walinda usalama wa Umoja wa Mataifa, wamekuwa wakisaidiana na wanajeshi wa DRC kupambana na makundi ya waasi.
Walinda usalama wa Umoja wa Mataifa, wamekuwa wakisaidiana na wanajeshi wa DRC kupambana na makundi ya waasi. AP - Moses Sawasawa

Mapigano haya yameripotiwa ikiwa ni siku mbili tangu kikosi cha umoja wa Mataifa, MONUSCO kutangaza operesheni za pamoja na jeshi la Serikali inayofahamika kama Springbok, dhidi ya waasi hao na makundi mengine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.