Kenya: Ruto aonya mawaziri wanaochelewa kwenye vikao
Nairobi – Nchini Kenya, Rais William Ruto ameelezea kuchukizwa na hatua ya kuchelewa kwa baadhi ya mawaziri wake wakati wa kikao cha baraza la mawaziri mapema leo Jumanne katika Ikulu ya Nairobi na kuwataka waliochelewa kuwasilisha maelezo kwa maandishi.
Imechapishwa:
Rais Ruto amekuwa akiongoza hafla ya kutia saini kandarasi za utendakazi kwa maofisa wake ambapo baadhi walichelewa kuwasili kama ilivyokuwa imeratibiwa.
Miongoni mwa wale walioripotiwa kuchelewa kufika kwenye kikao ni pamoja na waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki na waziri wa biashara Moses Kuria ambao hawakushiriki kwenye hafla hiyo kutia saini kandarasi za utendakazi.
Mkuu wa nchi ameeleza kuwa viongozi waliopewa jukumu la kuwatumikia raia wa Kenya wanapaswha kufanya kazi kwa uadilifu.
"If you cannot keep time with your employer you have basically dismissed yourself"
— NTV Kenya (@ntvkenya) August 1, 2023
President Ruto asks members of the Executive who arrived late at Cabinet Appraisal meeting, to submit written explanations. pic.twitter.com/0nLI3TQ1vx
Ruto ambaye alionekana na kukerwa alisisitiza kuwa anashikilia kwa dhati masuala yanayohusiana na utoaji huduma na yeyote anayeshughulikia masuala ya kitaifa bila kujali atawajibishwa.
Kandarasi wa utendakazi serikalini zinatumika kama kigezo cha kupima utendakazi wa wizara na mashirika katika kuwahudumia Wakenya.
Aidha mkuu wa nchi amewaonya maofisa wa umma dhidi ya kujihusisha na vitendo vya ufisadi na kuwataka kuwajibikia majukumu yao.
Aliwakosoa mawaziri ambao mara kwa mara walisafiri nje ya nchi, na kuzuia utendakazi wa kamati za baraza la mawaziri.
“I have been late in your meeting one day only and I was embarrassed,” DP Gachagua says as President Ruto locks out late CSs pic.twitter.com/xvRXlvMiTb
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) August 1, 2023
Naibu rais Rigathi Gachagua naye pia amewataka mawaziri kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia muda.