Pata taarifa kuu

Kenya: Maandamano ya upinzani yaingia siku ya pili, watu sita wakiripotiwa kuuawa

Watu sita wameripotiwa kupoteza maisha katika maandamano ya siku tatu yaliyoanza Jumatano ya wiki hii nchini Kenya, kupinga kile upinzani unasema ni kupanda kwa gharama ya maisha, huku wizara ya mambo ya ndani ikithibitisha kukamatwa kwa waandamanaji zaidi ya 300.

Maandamano ya upinzani yanaingia siku ya pili
Maandamano ya upinzani yanaingia siku ya pili REUTERS - THOMAS MUKOYA
Matangazo ya kibiashara

Katika mitaa yenye wafuasi wengi wa upinzani kama Mathare na Kibera jijini Nairobi, polisi walitumia vitoza machozi kuwasambaratisha waandamanaji, huku kukiwa na ripoti ya baadhi watu waliojitkeza kuandamana wakijeruhiwa kwa kupigwa risasi.

Polisi wanasema maandamano hayo hayakubaliki
Polisi wanasema maandamano hayo hayakubaliki REUTERS - JOHN MUCHUCHA

Katika mwa jiji la Nairobi, athari za maandamano zimeshuhudiwa, maduaka yalifungwa na kinyume na siku nyingine hapakuwa na msongamano wa magari.

“Kwa kweli hakuna kitu tumeuza kwa sababu hakuna mtiririko wa watu.” Alisema Abadalla raia wa Kenya.

00:04

Abdalla, raia wa Kenya kuhusu maandamano

Baadhi ya raia wameonekan kuunga  mkono maandamano haya huku wengine wakipinga.

Polisi wanasema wamewakamata karibia waandamanaji 300
Polisi wanasema wamewakamata karibia waandamanaji 300 REUTERS - THOMAS MUKOYA

“Hatuwezi zungumza maneno ya serikali wakati ambapo hata mwaka moja haujaisha, tusubiri mwaka ukamilike ndiyo tuone matokeo yake.” alisema mmoja wa wakaazi wa Nairobi.

00:10

Raia wa Kenya kuhusu maandamano

Maandamnao hayo yanaendelea tena hii leo Alhamis na kesho Ijumaa na muungano wa upinzani Azimio la Umoja, katika taarifa yake iliyotiwa saini na Martha Karua, naibu kiongozi wa muungano huo ameshtumu polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji na kuwakamata baadhi ya viongozi wa upinzani, wakiwemo wabunge.

George Ajowi- RFI-Kiswahili Nairobi

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.