Pata taarifa kuu

Kenya: Shughuli za kibiashara zimeonekana kutatizika katika baadhi ya miji

Maafisa wa polisi wa kupambana na ghasia wameonekana  katika maeneo tofauti ya mji mkuu wa Kenya kabla ya maandamano ya kuipinga kupanda kwa gharama ya maisha yaliopangwa na  upinzani katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

Biashara zimeonekana kutatizika katika baadhi ya miji nchini Kenya kuelekea maandamano ya upinzani
Biashara zimeonekana kutatizika katika baadhi ya miji nchini Kenya kuelekea maandamano ya upinzani REUTERS - MONICAH MWANGI
Matangazo ya kibiashara

Picha zilizochapishwa na  vyombo vya habari vya ndani zimeonyesha vizuizi  vya barabarani vikiwa vimewekwa katika maeneo tofauti ya jiji kuu Nairobi.

Shughuli za kibiashara katikati mwa jiji kuu zimeonekana kutatizika, maduka mengi tu yakiwa yamefungwa wakati baadhi ya magari ya uchukuzi wa umma yakionekana kuwa machache ikilinganishwa na siku nyengine.

Mjini Kisumu, barabara mbalimbali zimefungwa na waandamanaji ambao wameonekana wakiwa wamewasha moto magurudumu ya magari ,Maduka pia yamefungwa usafiri wa umma ukionekana kutatizika.

Maafisa wa polisi tayari wametumwa katika maeneo muhimu karibu na mji huo, upinzani ukisisitiza utaendelea na maadamano yake kama ilivyopangwa.

Polisi wametumwa kuwakabili waandamanaji katika baadhi ya miji
Polisi wametumwa kuwakabili waandamanaji katika baadhi ya miji REUTERS - THOMAS MUKOYA

Hali sawa na hiyo pia imeshuhudiwa katika mji wa Migori ambapo shughuli za uchukuzi zimeathirika wakati  biashara zikiwa zimefungwa, idadi kubwa ya maofisa wa polisi wakionekana wakipiga doria.

Maeneo ya Kitengela, kaunti ya Kajiado ambapo maandamano ya vurugu yalishuhudiwa wakati wa maandamano ya awali, maofisa wa polisi wametumwa huko pia,  shughuli ndogo za kibiashara zikiendelea.

Katika maeneo mengine, polisi wamewakamata baadhi ya watu waliokuwa wamejitokeza kuaandamana.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.