Kenya: Upinzani na serikali zatakiwa kutatua changamoto zao kwa amani
Nairobi – Wajumbe kutoka nchi za Marekani, Uingereza , Canada ,Ujerumani na mataifa mengine tisa wameeleza kuguswa na machafuko na vifo vilivyoripotiwa wakati wa maandamano ya kupinga kupanda kwa gharama ya maisha nchini Kenya.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mabalozi hao kumi na watatu wametoa wito kwa pande husika katika mzozo huo kutatua changamoto zao kwa njia ya amani.
Wito huu unakuja wakati huu upinzani kupitia hotuba yake kwa vyombo vya habari nchini humo ukisisitiza kuendelea na maandamano yao ya siku tatu licha ya serikali kuonya kwamba hatafanyika.
The UK joins 🇦🇺🇨🇦🇩🇰🇫🇮🇩🇪🇮🇪🇳🇱🇳🇴🇸🇪🇨🇭🇺🇦 🇺🇸 in expressing concern at the violence seen during last week's demonstrations - and in calling for parties in Kenya to work to find a constructive and peaceful solution.
— UK in Kenya 🇬🇧🇰🇪 (@UKinKenya) July 18, 2023
--
Read more: https://t.co/ghrCMxGYRn pic.twitter.com/ik5PUw9aqw
Katika taarifa yao, mabalozi hao wamesema kwamba wanatambua changamoto zinazowakabili raia katika taifa hilo la Afrika Mashariki na kwamba wanatoa wito kwa serikali na upinzani kuweka matakwa yao wazi ilikupata suluhu ya kuendeleza nchi hiyo.
Serikali ya Nairobi imesisitiza kwamba haitaruhusu kufanyika kwa maandamano mengine yenye vurugu, upinzani ukisema wafuasi wake hawafanyi maandamano yenye vurugu.