Pata taarifa kuu

Kenya: Watu 300 wamekamatwa kwa kushiriki maandamano ya upinzani

Nairobi – Nchini Kenya, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema zaidi ya watu 300, ikiwa ni pamoja na mbunge mmoja wamekamatwa kufuatia maandamano ya kulalamikia kupanda kwa gharama ya maisha yaliyoharamishwa na polisi na kusababisha vifo vya watu saba na kuwaacha wengine nba majeraha. 

Polisi wanasema wamewakamata watu 300 wanaohusishwa na maandamano hayo yaliogeuka kuwa machafuko
Polisi wanasema wamewakamata watu 300 wanaohusishwa na maandamano hayo yaliogeuka kuwa machafuko REUTERS - THOMAS MUKOYA
Matangazo ya kibiashara

Baada ya maandamano hayo yaliyotishwa na upinzani na kugeuka kuwa ya vurugu kati ya waandamanaji na polisi, shughuli za kawaida zimeanza kurejelewa tena.  

Shughuli za kibiashara zilitatizika wakati wa maandamano hayo
Shughuli za kibiashara zilitatizika wakati wa maandamano hayo REUTERS - THOMAS MUKOYA

Hawa ni baadhi ya Wakenya waliorejelea majukumu yao baada ya maandamano ya jana. 

“Mimi hufanya kazi ya kuweka magari vidhibiti mwendo lakini wakati wa maandamano hata sikwenda kazi hilo limeniumiza sana.” Walisema baadhi ya raia wa taifa hilo.

00:31

Baadhi ya raia wa Kenya waliorejelea majukumu yao

Watetezi wa haki za binadamu, wamewashtumu polisi kwa kutumia nguvu kupita kisiasa kukabiliana na waandamanaji. 

Polisi wanasema hawataruhusu maandamano kufanyika tena
Polisi wanasema hawataruhusu maandamano kufanyika tena REUTERS - BRIAN OTIENO

Samson Omondi .ni kutoka Shirika la kutetea haki za binadamu nchini Kenya-KHRC. 

“Kumekuwa na ukiukaji wa haki za binadamu kutokana na namna maofisa wa polisi walitumia nguvu wakati wa maandamano.” Samson Omondi, mtetezi wa haki za binadamu nchini kenya.

00:14

Samson Omondi, Mtetezi wa haki za binadamu nchini kenya

Naibu rais Rigathi Gachagua amemhstumu kiongozi wa upinzani Raila Odinga kwa maafa na uharibu uliofanyika. 

“Huyu ndiye anatuletea shida nchini Kenya na matatizo yetu yataisha iwapo tutamalizana naye.”alisema naibu wa raisRigathi Gachagua.

00:08

Naibu rais Rigathi Gachagua

Odinga amesisitiza kuwa ataitisha maandamano zaidi katika siku zijazo, hadi pale rais William Ruto atakapokubali kupunguza gharama ya maisha miongoni mwa mambo mengine. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.