Pata taarifa kuu

Kenya: Polisi wanakabiliana na waandamanaji katika maeneo tofauti

Nairobi – Waandamanaji wa upinzani nchini Kenya wameendelea na maandamano yaliyopangwa siku ya Jumatano, kukaidi onyo kutoka kwa polisi walioyataja maandamano hayo kuwa haramu.

Raia katika maeneo mbalimbali nchini Kenya yameripoti maandamano ya raia wanaopinga kupanda kwa gharama ya maisha
Raia katika maeneo mbalimbali nchini Kenya yameripoti maandamano ya raia wanaopinga kupanda kwa gharama ya maisha AP - Samson Otieno
Matangazo ya kibiashara

Polisi wametumia vitoa machozi kuwatawanya waandamanaji katika miji mbalimbali huku mkuu wa polisi akisema ni sharti hatua muhimu zichukuliwe ili kuwatawanya.

Shughuli za kibiashara zilitatizika wakati wa maandamano hayo
Shughuli za kibiashara zilitatizika wakati wa maandamano hayo REUTERS - THOMAS MUKOYA

Waandalizi wa maandamano wanatoa wito wa kufutwa kwa sheria mpya ambayo inaongeza maradufu ushuru wa mafuta na kuweka ushuru wa nyumba wa 1.5% kwa wafanyikazi. Kwa sasa imesitishwa na mahakama kuu jijini Nairobi, kwa sababu ya masuala ya kikatiba.

Lakini serikali inasema hatua hiyo ni muhimu kurekebisha masuala ya ulipaji wa deni na kuunda nafasi za kazi kwa vijana wasio na ajira.

Maeneo mbalimbali yalisitisha biashara wakati wa maandamano ya upinzani
Maeneo mbalimbali yalisitisha biashara wakati wa maandamano ya upinzani REUTERS - THOMAS MUKOYA

Ijumaa iliyopita, makabiliano kati ya waandamanaji wa upinzani na polisi yalisababisha vifo vya watu sita katika miji mingi.

Siku ya Jumatano, barabara kuu katika jiji kuu la Nairobi pamoja na Kisii, Kisumu na Nyeri hazina shughuli nyingi, na video za mtandaoni zinaonyesha barabara zilizofungwa katika maeneo kadhaa. Madereva wa mabasi na teksi wamejiunga na maandamano hayo, wakielezea wasiwasi wao kuhusu kupanda kwa gharama ya mafuta.

Mtu mmoja ameripotiwa kufariki katika maandamano ya leo baada ya kupigwa risasi kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Baadhi ya miundo mbinu ikiwemo barabara zimeharibiwa.

Kando na hayo, picha zilizosambazwa mitandaoni zimeonyesha gari la polisi likiwa limechomwa moto katika maandamano ya leo. Biashara nyingi zimesalia kufungwa, na usafiri umesimama.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.