Kenya: Wanaharakati waliokuwa wamekusanyika nje ya kituo cha polisi wametawanywa
Nairobi – Maofisa wa polisi jijini Nairobi wamewatawanya watetezi wa haki za binadamu nchini humo waliokuwa wamefika katika kituo cha polisi cha Central wakitaka kuachiwa kwa wenzio waliokamatwa wakati wa maandamano ya Ijumaa dhidi ya serikali.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa picha na video zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii, wanaharakati hao wameonekana wakitwanya na walinda usalama kwa mabomu ya machozi wakati wengine wakikamatwa.
Jaji mkuu wa zamani wa Kenya Dkt Willy Mutunga ni miongoni mwa waandamanaji waliokuwa wamejitokeza kushinikiza polisi kuwachia wanaharakati hao wanaoshikiliwa katika kituo hicho.
Human rights activists among them Former Chief Justice Willy Mutunga dispersed by police as they attempted to protest inside the Central Police Station pic.twitter.com/nSr0Vgg319
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) July 8, 2023
Bonfence Mwangi, mwanaharakati mashuhuri nchini humo kupitia mitandao yake ya kijamii amewataka viongozi wa upinzani Raila Odinga na Martha Karua kushinikiza kuachiwa kwa watu hao ambao walikuwa miongoni mwa Wakenya waliojitokeza kuitikia wito wao wa kuandamana.
Maelfu ya raia katika taifa hilo la Afrika Mashariki waliandamana siku ya Ijumaa ya wiki hii katika maeneo mbalimbali kulalamikia kupanda kwa gharama ya maisha pamoja na ushuru unaongeza bei ya bidhaa za petroli.
Mtu mmoja amewauwa kwa kupigwa risasi huku wengine wengi wakiwa wamejeruhiwa ,wakati wa maandamano ya saba saba nchini Kenya ,yaliyoongozwa na kinara wa upinzani Raila Odinga ,kupinga gharama ya juu ya maisha.
36 comrades from @sjustice_tt and @UhaiWetu are being illegally detaining at Central PoliceStation. Theyneed food & urgent medical care because theyhave been seriously brutalised. Solidarity needed urgently. @WMutunga @thekhrc @IMLU_org @katibainstitute @HakiKNCHR @DefendersKE pic.twitter.com/xKxjOmm810
— Social Justice Travelling Theatre (@sjustice_tt) July 7, 2023
Raila akizungumzwa wakati wa maandamano hayo ambayo msafara wake ulishambuliwa na maofisa wa polisi ,amesema matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola ,hayatamaliza juhudi za upinzani kutetea maslahi ya raia.
Muungano wa upinzani, wa Azimio la Umoja ,umesema kuwa maandamano hayo yataendelea jumatano wiki ijayo huku muungano huo ukiendelea na ukusanyaji wa saini milioni moja kufanikisha kura ya maoni ya kutaka kuondolewa wa utawala wa Kenya Kwanza wake rais Ruto.