Kenya: Odinga anaongoza wafuasi wake kupinga kupanda kwa gharama ya maisha
Nairobi – Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga, ameongoza mkutano wa kisiasa katika uwanja wa kihistoria wa Kamkunji jijini Raila kupinga kile wanachosema ni kupanda kwa gharama ya maisha ambapo pia amewataka wafuasi wake kuandamana hadi katika jiji kuu.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Maofisa wa polisi wameonekana katika miji mbalimbali ya taifa hilo kuwakabili waandamanaji waliojitokeza kuitikia wito wa kiongozi wa upinzani kuandamana kupinga sheria tata inyaopendekeza kupanda kwa ushuru wa bidhaa.
Katika kaunti ya Mombasa, pwani ya taifa hilo la Afrika Mashariki, polisi wametawanya kwa vitoa machozi waliokuwa wamekusanyika kwenye maeneo tofauti katika kaunti hiyo.
Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga na muungano wake wa Azimio wamekuwa namkutano jijini Nairobi kabla ya kuanza maandamano dhidi ya serikali kulalamikia sheria hiyo mpya wanayodaiwa inawaongezea mzigo raia ambayo tayari wanakabiliwa na changamoto za kimaisha.
"Kuna njia nyingi za kuenda Huruma. Wakizuia hapa, mnapita pale." Azimio leader Raila Odinga urges supporters attending Saba Saba rally at Kamukunji to us alternative routes as they hold #Maandamano pic.twitter.com/tPh5k7jYLq
— KTN News (@KTNNewsKE) July 7, 2023
"Rais William Ruto anatutoza ushuru bila idhini yetu na kutunga sheria ambazo matokeo yake ni kufanya maisha kuwa magumu," Azimio ilisema kwenye taarifa iliyotolewa mapema wiki hii.
Ruto wiki jana alitia saini kuwa sheria mswada wa fedha ambao unatarajiwa kusaidia serikali yake kupata zaidi ya dola bilioni 2.1 kwa hazina ya serikali iliyopungua na kusaidia kukarabati uchumi wa taifa hilo unaokabiliwa na madeni makubwa.
Tofauti na iliyokuwa kwa maandamano ya awali, wakati huu yameonekana kufanyika katika baadhi ya maeneo ya mishinani.
Wajackoyah, Oparanya and Wamalwa leading protests caravan in Luanda Market in Vihiga. pic.twitter.com/mGfy2SgbwM
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) July 7, 2023
Sheria hiyo ya fedha imeongeza ushuru mpya au ongezeko la bidhaa mbalimbali za kimsingi kama vile mafuta na chakula na uhamishaji wa pesa kwa njia ya simu, pamoja na ushuru wenye utata kwa Wakenya wote wanaolipa ushuru kufadhili mpango wa makazi yenye bei nafuu.
Mahakama kuu jijini Nairobi Ijumaa iliyopita ilisitisha utekelezaji wa sheria hiyo baada ya seneta wa Busia, Magahribi ya taifa hilo Okiya Omutata kuwasilisha kesi kupinga uhalali wake wa kikatiba.
.@RailaOdinga: Tulisema kila kitu chenye tutafanya kitakuwa kwa njia ya amani. Tumewambia polisi hatutaki fujo. Hatuaribi maali ya watu wengine. Tutatoika hapa kwa amani.#K24Siasa pic.twitter.com/6bwuPoMRCV
— K24 TV (@K24Tv) July 7, 2023
Licha ya uamuzi huo, bodi ya kudhibiti nishati nchini Kenya baadaye siku hiyo ilitangaza kupanda kwa bei ya mafuta ili kuzingatia kuongezeka kwa ushuru wa hadi asilimia 16 kama ilivyoainishwa katika sheria hiyo yenye utata.
Maandamano hayo yamepewa jina la "Saba Saba" huku yakifanyika siku ya saba ya mwezi wa saba.