Pata taarifa kuu

Kenya: Upinzani umesisitiza msimamo wake kupinga muswada wa fedha wa 2023

NAIROBI – Wakati huu wabunge nchini Kenya, wakisubiri kusomwa mara ya tatu kwa muswada wa fedha ulioibua mjadala miongoni mwa raia na wadau nchini humo, muungano wa upinzani umesisitiza msimamo wake kupinga muswada huo inaosema utawaumiza wananchi.

Viongozi wa upinzani nchini Kenya wamesisitizia msimamo wao wa kupinga muswada wa fedha wa mwaka wa 2023
Viongozi wa upinzani nchini Kenya wamesisitizia msimamo wao wa kupinga muswada wa fedha wa mwaka wa 2023 © Raila Odinga
Matangazo ya kibiashara

Muswada huu ulijadiliwa na kusomwa mara ya pili hapo jana Jumatano, ambapo wabunge walivutana kuhusu baadhi ya vipengele, licha ya Serikali kukubali kufanya marekebisho katika baadhi ya sehemu za muswada huo.

Miongoni mwa vipengele vinavyopingwa ni pamoja na kodi ya ujenzi wa makazi nafuu, nyongeza ya kodi katika mafuta na bidhaa nyingine ambazo zinamgusa mwananchi moja kwa moja, Serikali hata hivyo ikisisitiza muswada huo lazima upitishwe.

Martha Karua, ni mwanasiasa kutoka muungano wa upinzani wa Azimio.

“Hakuna wakati Azimio imewatishia wabunge na baada ya bajeti hii ambayo ni rasimi haiuungwi mkono na Wakenya, azimio itachukua hatua zifaazo.” alisema Martha Karua.

00:34

Martha Karua- Mmoja wa viongozi wa upinzani nchini Kenya

Naye kiongozi wa muungano huo wa upinzani, Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga anasema atawaongoza raia katika taifa hilo la Afrika Mashariki  kupinga kupitishwa kwa Mswada wa Fedha wa 2023 .

Akizungumza wakati alipozuru soko la Toi katika eneo bunge la  Kibra, jijiini Nairobi ambalo lilibomolewa lilichomeka mapema wiki hii, kiongozi huyo alikashifu masuala muhimu katika Mswada huo ikiwa ni pamoja na asilimia 16 ya ushuru wa bidhaa za petroli, ushuru wa nyumba, na fidia ya bima.

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga © Raila Odinga

Upinzani umetoa wito kwa serikali kuaanzisha mazungumzo ya kitaifa kujadili kuhusu ushuru tata wa nyumba kwa nia ya kuwashawishi Wakenya kuunga mkono ajenda badala ya kuwashurutisha wafanyikazi na waajiri kulipa ushuru huo wa asilimia 1.5.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.