Kenya: Odinga aitaka serikali kuachana na muswada wa fedha wa 2023
NAIROBI – Nchini Kenya, kiongozi Azimio la Umoja Raila Odinga ameongeza shinikizo kwa rais William Ruto akimtaka kuachana na mapendekezo ya muswada wa fedha wa mwaka wa 2023.
Imechapishwa:
Mwanasiasa huyo mkongwe, ametoa wito kwa rais Ruto kuachana na mpango huo anaosema unalenga kuwaongezea wakenya mzigo haswa wakati huu wanapokabiliwa na hali ngumu ya maisha.
Muungano wa Azimio umetishia kutumia njia zengine ambazo zitawahusisha raia ikiwemo maandamano, iwapo rais Ruto atawashawishi wabunge kuunga mkono muswada huo.
No regime has imposed so many high taxes on our people in return for nothing except fantasies and fairy tales. This Bill is economic sabotage.
— Raila Odinga (@RailaOdinga) June 8, 2023
If Ruto insists on this Bill, this country will go into full recession. This Bill requires and must get fierce resistance. pic.twitter.com/rC9buuJikT
Aidha katika hatua nyingine Odinga, ameishauri Serikali kupunguza ukubwa wa serikali, kuziba mianya inayochangia kupotea kwa fedha za umma, kupunguza safari za watumishi nje ya nchi, kupunguza marupurupu ya mawaziri na makatibu katika wizara.
Hizi majuzi rais Ruto alisema anasubiri kuona wabunge watakaopinga muswada huo, hatua ambayo wachambuzi wa siasa wanasema inalenga kuwashurutisha.