Pata taarifa kuu

Kenya: Polisi waonekana katika barabara za Nairobi kudhibiti maandamano

NAIROBI – Nchini Kenya, idadi kubwa ya maofisa wa polisi wa kupambana na ghasia wametumwa katika maeneo tofauti ya jiji kuu la Nairobi wakati huu upinzani nchini humo ukiitisha maandamano ya nchi nzima kupinga kile wanachosema ni kupanda kwa bei za bidhaa pamoja na masula mengine yakiwemo yanayohusu tume ya uchaguzi IEBC.

Maofisa wa polisi wa kupamabana na ghasia jijini Nairobi, Kenya Mei 2, 2023. REUTERS/Thomas Mukoya
Maofisa wa polisi wa kupamabana na ghasia jijini Nairobi, Kenya Mei 2, 2023. REUTERS/Thomas Mukoya REUTERS - THOMAS MUKOYA
Matangazo ya kibiashara

Licha ya hayo, hali ya kawaida imeshuhudiwa katikati mwa jiji kuu la Nairobi japokuwa maeneo mengi ya biashara yamesalia kufungwa baadhi wakihofiwa kuwa huenda biahsara zao zikaporwa wakati wa maandamano hayo.

Idadi kubwa ya maofisa wa polisi pia imeshuhudiwa katika majengo ya tume ya uchaguzi IEBC, na majengo mengine ya serikali yaliokatikati mwa jiji kuu ambayo upinzani katika taarifa yake ulisema utazuru kupeleka lalama zao kwa wahusika.

Katika barabara ya Ngong, nje na jiji kuu la Nairobi, basi la abiria limeripotiwa kuchomwa moto kwa mujibu wa picha zilizochapishwa na vyombo vya habari vya ndani, watu waliokuwa wanataka kuaandamana wakidaiwa kuhusika na tukio hilo.

Maofisa wa polisi jijini Nairobi wakiwa kando na gari linalodaiwa kuchomwa na waandamanaji
Maofisa wa polisi jijini Nairobi wakiwa kando na gari linalodaiwa kuchomwa na waandamanaji REUTERS - THOMAS MUKOYA

Tangu saa kumi na mbili na nusu kwa saa za Afrika Mashariki, vizuizi vya polisi vilionekana kuekewa katika barabara inayoelekea katika ofisi za Ikulu, huku maafisa wa polisi wakionekana katika barabara zinazoelekea kwenye Ikulu ya Nairobi.

Kando na Nairobi, maeneo mengine kama vile kaunti ya Kisumu, waandamanaji wameonekana wakiwa barabara kuitikia wito wa kiongozi wao, matairi ya magari yakiwa yamewashwa barabarani.

Polisi katika mji wa Kibera jijini Nairobi wakiondoa matairi yaliochomwa moto na waandamanaji
Polisi katika mji wa Kibera jijini Nairobi wakiondoa matairi yaliochomwa moto na waandamanaji AP - Samson Otieno

Maandamano ya leo Jumanne yanakuja wakati huu mkuu wa polisi jijini Nairobi Adamson Bungeiakiwa ameyaharamisha kwa msingi kuwa maandamano ya awali yaligeuka kuwa vurugu.

Licha ya polisi kukataa kutoa kibali cha kufanyika kwa maandamano hayo ya upinzani, Kinara wa Azimio la Umoja, Raila Odinga amesisitiza kuwa yatafanyika kama ilivyopangwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.