Pata taarifa kuu

Kenya: Huenda mazungumzo kati ya upinzani na serikali yakagonga mwamba

NAIROBI – Nchini Kenya, ni wazi sasa  huenda mazungumzo kati ya upinzani na Serikali yakagonga mwamba, baada ya kauli za hapo jana za rais William Ruto na  kinara wa Azimio, Raila Odinga.

L'ancien Premier ministre et chef de l'opposition kenyane Raila Odinga (à gauche) et l'ancien vice-président et candidat à la présidence de l'alliance Kenya Kwanza William Ruto (à droite).
L'ancien Premier ministre et chef de l'opposition kenyane Raila Odinga (à gauche) et l'ancien vice-président et candidat à la présidence de l'alliance Kenya Kwanza William Ruto (à droite). AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Ruto sasa anamtaka kiongozi huyo kukubaliana na mchakato wa kibunge kupata suluhu au vinginevyo asubiri uchaguzi wa mwaka 2027.

"Nyinyi kama viongozi twendeni kule bunge tukaongee maneno ya viongozi  kupitia bunge. Hakuna haja ya kuharibu biashara ya mwanachi."amesisitiza rais William Ruto.
00:19

Rais wa Kenya William Ruto kuhusu Mazungumzo

Ni kauli ambayo hata hivyo haikupokelewa vizuri na Odinga, ambaye anasisitiza mchakato wa kibunge lazima uwe kwanza nje ya bunge, akitishia kuitisha tena maandamano ikiwa Serikali itashikilia msimamo wake.

"Tunasukumwa na wasiwasi kwamba licha ya katiba ya mwaka wa 2010, utamaduni wetu wa kisiasa unabaki kuwa mshindi ana mamlaka ya kila kitu, hii ndiyo imejitokeza wazi katika utawala uliopita."ameeleza Raila Odinga, kinara wa upinzani nchini Kenya.
00:22

Raila Odinga, Kinara wa upinzani nchini Kenya kuhusu mazungumzo

Haya yanajiri baada ya juma lililopita, Odinga kutangaza kusitisha maandamano ya Jumatatu na Alhamisi, kuitikia wito wa rais Ruto kuhusu mazungumzo ya kupata suluhu.

Wito umekuwa ukitolewa kwa viongozi hawa wawili wa kisiasa kuketi pamoja na kutafuta suluhu la mvutano kama njia moja ya kuepusha taifa hilo kuingia katika machafuko ya kisiasa.

Suala la misimamo mikali kati ya mrengo wa Odinga na upande wa serikali ya rais Ruto likiajwa kuwa kizingiti kikubwa kwa kukwamisha mazungumzo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.