Pata taarifa kuu
DRC-USALAMA

Serikali ya DRC na makundi ya waasi kukutana Nairobi

Kenya itakuwa mwenyeji wa mazungumzo kati ya makundi ya waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na serikali ya Kinshasa

Rais Uhuru Kenyatta (wa pili kulia) na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi (kushoto) wakiangalia ramani mpya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kutia saini mkataba wa kuiunganisha DRC katika jumuiya ya kibiashara ya Afrika Mashariki, jijini Nairobi mnamo Aprili 8, 2022.
Rais Uhuru Kenyatta (wa pili kulia) na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi (kushoto) wakiangalia ramani mpya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kutia saini mkataba wa kuiunganisha DRC katika jumuiya ya kibiashara ya Afrika Mashariki, jijini Nairobi mnamo Aprili 8, 2022. AFP - TONY KARUMBA
Matangazo ya kibiashara

Hili limeafikiwa baada ya mkutano wa viongozi wa nchi za Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kukutana siku ya Alhamisi jijini Nairobi, kujadili hali ya usalama mashariki mwa DRC.

Baada ya mkutano huo, serikali ya DRC ikiongozwa na rais Felix Tshisekedi, inatarajiwa kukutana na makundi ya waasi jijini Nairobi hivi leo.

Mazungumzo haya yanakuja karibu mwezi mmoja baada ya DRC kujumuishwa kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aidha,  viongozi wa nchi hizo pia wamekubaliana kuangalia uwezekano wa kuunda jeshi la pamoja kukabiliana na makundi ya waasi iwapo yataendelea na harakati zao Mashariki mwa DRC.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.