Mechi za AFCON kuanza leo nchini Ivory Coast
Nairobi – Michuano ya soka kuwania taji la mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON, inaanza leo nchini Cote Dvoire. Hii ni mara ya kwanza kwa mashindano haya makubwa kurejea kwenye nchi hiyo ya Afrika Magharibi kwa mara ya kwanza baada ya miaka 40.
Imechapishwa:
Ni saa za kuhesabu hapa Abidjan , kabla ya kuanza kwa mechi ya ufunguzi kati ya wenyeji Coite Dvoire na Guinea-Bissau kwenye uwanja wa Allasane Outtara.
🤩 𝗣𝗶𝘁𝗰𝗵 is 𝓟𝓮𝓻𝓯𝓮𝓬𝓽.
— Total Energies AFCON (@TotalAFCON2023) January 13, 2024
🏟️ 𝗦𝘁𝗮𝗱𝗶𝘂𝗺 is 𝓢𝓽𝓾𝓷𝓷𝓲𝓷𝓰.
Everything is ready for the #TotalEnergiesAFCON2023 opener. Are you? 👀 pic.twitter.com/J6ZDadClrX
Kuanzia mapema leo, mashabiki wa soka, hasa wa hapa Cote Dvoire walianza kufurika uwanjani, kuishabikia timu yao, iliyoshinda mara mwisho taji hili mwaka 2015.
The wait is over! 🚨#TotalEnergiesAFCON2023 matchday 1 timings for you 👇 pic.twitter.com/50zqxsZbe7
— Total Energies AFCON (@TotalAFCON2023) January 13, 2024
Serikali ya Cote Dvoire, imewahakikishia usalama wageni wote waliokuja kutazama michuano hii, na maafisa wa polisi na wanajeshi zaidi ya Elfu 17 wanatumiwa kuhakikisha kuwa kila kitu kinaenda kama ilivyopangwa.
Mbali na hapa Abidjan, michuano hii itakayomalizika Februari 11, inachezwa pia kwenye jiji kuu Yamoussoukro, Bouake, mji wa Pwani wa San Pedro, Korhogo uliopo Kaskazini.
Knock Knock 🚪✊
— Total Energies AFCON (@TotalAFCON2023) January 13, 2024
Who’s there? 🤔
IT’S THE #TotalEnergiesAFCON2023 ! 😍
pic.twitter.com/3zMV6NwIAd
Kuna timu 24 zinazotafuta ubingwa wa taji hili, ikiwemo Taifa Stars ya Tanzania na Leopard ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoka Afrika Mashariki na Kati.
Jason Sagini, Abidjan, RFI Kiswahili