Pata taarifa kuu
COTE D'IVOIRE-BLE GOUDE-HAKI

Mahakama ya Cote d'Ivoire yamhukumu kifungo cha miaka 20 Charles Ble Goude

Kiongozi wa zamani wa kisiasa nchini Cote d'Ivoire Charles Ble Goude amesema amehukumiwa jela miaka 20 kwa makosa ya mauaji, ubakaji na mateso, hukumu aliyopewa akiwa nje ya nchi hiyo.

Charles Ble Goude ambale aliachiliwa kwa dhamana Hague, amehukumiwa na mahakama ya Cote d'Ivoire kifungo cha miaka 20 (picha ya kumbukumbu)
Charles Ble Goude ambale aliachiliwa kwa dhamana Hague, amehukumiwa na mahakama ya Cote d'Ivoire kifungo cha miaka 20 (picha ya kumbukumbu) Peter Dejong / POOL / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kabla ya hukumu hii Ble Goude ambaye alikuwa mshirika wa karibu rais wa zamani Laurent Gbagbo na kiongozi wa vijana katika chama tawala wakati huo nchini Cote d'Ivoire, alikuwa ameondolewa mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC.

Licha ya uamuzi huo wa ICC, serikali ya Cote d'Ivoire ilimfungulia mashtaka mapya dhidi yake, kwa madai ya kutekeleza tuhuma hizo wakati wa mzozo wa kisiasa kati ya mwaka 2010-2011.

Mwanasiasa huyo licha ya kuondolewa mashtaka, bado yupo nchini Uholanzi wakati huu ofisi ya kiongozi wa mashtaka katika Mahakama ya ICC ikitarajiwa kukataa rufaa.

Machafuko ya kisiasa nchini Cote d'Ivoire yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 3,000.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.