Pata taarifa kuu
USALAMA-ULINZI

Ukraine: Urusi yafanya mashambulizi kwenye bandari ya mkoa wa Odessa

Ndege kadhaa zisizo na rubani za Urusi zimeshambulia mji mkuu wa Ukraine Kyiv usiku wa Jumanne kuamkia Jumatano, na kusababisha uharibifu wa mali lakini hakuna majeruhi.

Ulinzi wa anga wa Ukraine waizuia ndege isiyo na rubani ya Shahed iliyokuwa ikiruka wakati wa shambulio la tatu la anga la Urusi kwenye mji mkuu Kyiv, Ukraine, Mei 30, 2023.
Ulinzi wa anga wa Ukraine waizuia ndege isiyo na rubani ya Shahed iliyokuwa ikiruka wakati wa shambulio la tatu la anga la Urusi kwenye mji mkuu Kyiv, Ukraine, Mei 30, 2023. AP - Evgeniy Maloletka
Matangazo ya kibiashara

Shambulio la ndege zisizo na rubani pia limefanyika usiku kusini mwa mkoa wa Odessa, bandari kuu ya Ukraine kwenye Bahari Nyeusi. Moto unaendelea. Fuata matukio ya hivi punde katika vita vya Ukraine saa baada ya saa.

Shambulio la ndege zisizo na rubani za Urusi limeharibu miundombinu ya bandari na kusababisha moto mkubwa katika jimbo la Odessa kusini mwa Ukraine, gavana wa eneo hilo Oleg Kiper ametangaza Jumanne usiku.

"Kutokana na shambulio hilo, moto ulizuka katika vituo vya bandari na miundombinu ya viwanda katika eneo hilo," Oleg Kiper ameandika kwenye Telegram. Hakuna majeruhi yalioripotiwa hapo awali.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.