Pata taarifa kuu

EAC: TotalEnergies kutathmini upya ununuzi wa ardhi kwa ujenzi wa bomba la mafuta

Nairobi – Kampuni ya mafuta ya Ufaransa TotalEnergies imetangaza mpango wa kutathmini upya ununuzi wa ardhi kwenye mradi wake wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Uganda kupitia nchini Tanzania, unaokosolewa na wanamazingira.

Uchimbaji visima ulianza katikati ya 2023 na uzalishaji unatarajiwa kuanza mnamo 2025
Uchimbaji visima ulianza katikati ya 2023 na uzalishaji unatarajiwa kuanza mnamo 2025 AFP - STEPHANE DE SAKUTIN
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kampuni hiyo kubwa ya mafuta ya Ufaransa TotalEnergies imesema kwamba ujumbe wake umepewa jukumu maalum katika kuhakikisha mapitio ya kila hati iliyoafikiwa na pande zote inauwiana na utafiti uliofanywa hivi karibuni katika nyanja ya ardhi ya miradi yake ya mafuta nchini Uganda na Tanzania, Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) na Tilenga, ambayo inakabiliw ana upinzani mkubwa kutoka kwa wanaharakati wa mazingira kutoka Uganda.

Kampuni ya TotalEnergies inaendelea na mradi wake wa kuchimba visima vya Tilenga nchini Uganda na Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) lenye urefu wa kilomita elfu moja mia nne arobaini na tatu linalosafirisha mafuta hadi pwani ya Tanzania.

Watetezi wa mazingira wamekuwa wanapinga mradi mradi huo kuwa si salama kwa mazingira
Watetezi wa mazingira wamekuwa wanapinga mradi mradi huo kuwa si salama kwa mazingira © REUTERS/Abubaker Lubowa

Taarifa ya Total Energies inasema kwamba Ujumbe wa maafisa wake utatathmini taratibu za utwaaji ardhi zilizotekelezwa, masharti ya mashauriano, fidia na uhamisho wa watu wanaohusika, na utaratibu wa kushughulikia malalamiko na kuongeza kuwa maafisa wake watawasilisha ripoti yao ifikapo mwezi Aprili mwaka huu.

Uchimbaji visima ulianza katikati ya 2023 na uzalishaji unatarajiwa kuanza mnamo 2025.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.