Pata taarifa kuu
UINGEREZA-MAFURIKO

Uingereza yakumbwa na mafuriko

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amewatembelea leo Jumatatu wakazi walioathirika na mafuriko kaskazini mwa Uingereza, mafuriko yaliotokana na mazingira ya hali isio kuwa ya kawaida, inayoathiri nchi kadhaa za Ulaya ya Magharibi.

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron (katikati) akipongeza askari wanaohusika na huduma ya dharura kwa wakazi wa mji wa  York, kaskazini mwa Uingereza, Desemba 28, 2015.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron (katikati) akipongeza askari wanaohusika na huduma ya dharura kwa wakazi wa mji wa York, kaskazini mwa Uingereza, Desemba 28, 2015. DARREN STAPLES/AFP
Matangazo ya kibiashara

Nchini Uhispania, joto kali lilio kwenye kiwango cha juu kuliko msimu wa wastani na kiwango cha chini cha mvua vimechangia kuondoka kwa majanga ya moto katika misitu.

Katika rasi ya Italia, shughuli kadhaa hususan magari yamepigwa marufuku kuingia barabarani katika miji mikubwa kadhaa kwa lengo la kupambana dhidi ya uchafuzi wa mazingira, unaosababishwa na kukosekana kwa mvua au upepo kwa muda wa wiki kadhaa.

Hali ambayo haijawahi kushuhudiwa kaskazini mwa Uingereza

Waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, amekutana mapema Jumatatu hii asubuhi na askari waliokua wakishiriki katika zoezi la uokoaji na ulinzi wa majengo katika mji wa York, katika kaunti ya Yorkshire (kaskazini), kwa mujibu wa maneno alioandika katika akaunti yake binafsi ya twitter.

Katika mji huo wa kihistoria wa York, majengo 500 yamekumbwa na mafuriko na magari kadhaa yamepelekwa na maji.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.