Pata taarifa kuu
UINGEREZA-UFARANSA-USHIRIKIANO

David Cameron ziarani Paris

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron anazuru jijini Paris nchini Ufaransa kukutana na rais François Hollande.

Waziri mkuu wa Ungereza, David Cameron anazuru Paris wiki zaidi ya moja baada ya kutokea kwa mashambulizi yaliogharimu maisha ya zaidi ya watu 130 jijini humo.
Waziri mkuu wa Ungereza, David Cameron anazuru Paris wiki zaidi ya moja baada ya kutokea kwa mashambulizi yaliogharimu maisha ya zaidi ya watu 130 jijini humo. REUTERS/Benoit Tessier
Matangazo ya kibiashara

Ni ziara inayokuja baada ya Islamic State kushambulia jiji la Paris na kuwauwa watu zaidi ya 130 na wengine kujeruhiwa.

Viongozi hao watajdiliana kuhusu namna ya kuimarisha usalama katika ya mataifa yao na kwingineko barani Ulaya.

Tayari Uingereza imesema kuwa inatarajia kutumia zaidi ya Dola bilioni 18 nukta 2 kuimarisha Wizara ya ulinzi na kupambana dhidi ya ugaidi kwa muda wa miaka mitano ijayo.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.