Pata taarifa kuu
MAREKANI-HALI MBAYA YA HEWA

Marekani: watu wasiopungua 44 wapoteza maisha kutokana na hali mbaya ya hewa

Vimbunga, mafuriko ya ghafla na theluji vimesababisha vifo vya watu wasiopungua 44 nchini Marekani tangu Jumamosi.

Nyumba kadhaa zimeharibiwa baada ya kimbunga kupiga katika mji wa Garland, Texas, Desemba 28, 2015 katika Garland Texas.
Nyumba kadhaa zimeharibiwa baada ya kimbunga kupiga katika mji wa Garland, Texas, Desemba 28, 2015 katika Garland Texas. AFP/AFP
Matangazo ya kibiashara

Hali hiyo imevuruga safari za ndege na shughuli zimezorota katika sekta ya uchukuzi wa magari katika kipindi hiki cha harakati kubwa kwa ajili ya siku kuu za mwisho wa mwaka.

Vimbunga vilipiga katika jimbo la Texas (kusini) mwishoni mwa wiki iliyopita na kuendelea Jumatatu wiki hii ikiwa ni pamoja na dhoruba kali za blizzard, mvua na mafuriko katika sehemu kubwa ya Marekani.

Mamilioni ya raia walikuwa wamekwama katika viwanja vya ndege Jumatatu hii baada ya safari 2,100 za ndege zilifutwa na zingine 3700 zikicheleweshwa, kulingana na mtandao wa shirika la ndege la FlightAware.

Hali mbaya ya hewa ilisababisha pia safari 1,640 za ndege kufutwa na zaidi 6,400 kucheleweshwa Jumapili, hasa kwa sababu ya mifumo ya dhoruba inayopiga kambi juu ya anga la jimbo la Texas.

Jumatatuhii jimbo la Chicago limekumbwa na hali mbaya ya hewa, ambapo kumeshuhudiwa dhoruba, vimbunga, mvua kali na mafuriko. Upepo mkali ulisababisha ndege 1,200 kukwama kwenye viwanja mbalimbali vya ndege.

Katika jimbo pekee la Texas watu 11 wamepoteza maisha kutokana na hali hiyo mbaya ya hewa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.