Pata taarifa kuu

Milio ya risasi imesikika Sudan kuelekea utekelezwaji wa mktaba  wa kusitisha vita

NAIROBI – Milio ya risasi na milipuko kwa mara nyingine imeshuhudiwa nchini Sudan hivi leo, saa chache kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mktaba  wa kusitisha mapigano kwa wiki moja ili kuruhusu misaada ya kibinadamu kuwafikia raia walio katika maeneo yalioathirika na vita hivyo.

Idadi kubwa ya raia wameripotiwa kutoroka mji wa Khartoum kutokana na mpigano yanayoendelea, 22 Mei 2023.
Idadi kubwa ya raia wameripotiwa kutoroka mji wa Khartoum kutokana na mpigano yanayoendelea, 22 Mei 2023. AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Makabliano haya mapya yanaripotiwa licha ya makubaliano kadhaa ya kusitisha mapigano ambayo yalikosa kuheshimiwa, ya hivi punde ikiwa mkabata ulioafikiwa kati ya pande mbili zinazopigana chini ya usimamizi wa Marekani na Saudi Arabia.

Kulingana na Marekani na Saudi Arabia, mkataba wa hivi punde ulioafikiwa siku ya Jumapili unafaa kuanza kutekelezwa Jumatatu ya wiki hii usiku ili kuruhusu misaada ya kibinadamu kuwafikia raia.

Siku ya Jumapili, pande hizo mbili zilitoa hakikisho la kuheshimu makubaliano haya mapya, hatua ambayo ilikaribishwa na  Umoja wa mataifa, umoja wa Afrika, Jumuiya za kikanda, Afrika mashariki na IGAD.

Licha ya makubaliano kadhaa ya usitishaji ya hapo awali kukosa kuheshimiwa, raia wa nchi hiyo walikuwa na matumaini kwamba mkataba huu mpya utatoa fursa ya kumaliza vita ambavyo vimeitikisa Khartoum na sehemu zingine nchini humo.

Takriban watu elfu 1 wameripotiwa kuuawa huku maelfu wakikimbia vita hvyo, wakati huu pia madaktari katika mji wa Khartoum wakionya juu ya kuanguka kwa mfumo wa afya jijini Khartoum.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.