Algeria: Saïd Bouteflika ahukumiwa kifungomiaka miwili
Shirika la habari la serikali la APS nchini algeria limebaini kwamba Saïd Bouteflika, mdogo hayati wa raisAbdelaziz Bouteflika, amehukumiwa na mahakama ya Algiers kifungo cha miaka miwili jela kwa kuzuia "mahakama kufanya kazi yake".
Imechapishwa:
Mwendesha mashtaka alikuwa ameomba miaka saba gerezani kwa "kughusi nyaraka rasmi" na "matumizi mabaya ya madaraka". Katika kesi hiyo, ofisi ya mashitaka inawashtaki maafisa wengine kadhaa wa utawala wa zamani nchini Algeria.
Saïd Bouteflika, mshauri wa zamani wa kaka yake, hayati rais Bouteflika, anazuiliwa jela tangu mwezi Mei 2019, wakati alipokamatwa pamoja na watuhumiwa wenzake watatu na kuhukumiwa kifungo cha miaka kumi na tano jela.