Pata taarifa kuu
NIGERIA-BOKO HARAM-USALAMA

Nigeria: watu 17 wauawa Yobe

Watu 17 wamepoteza maisha baada ya kutokea kwa mashambulizi matatu ya kujitoa mhanga katika jimbo la Yobe.

Askari wa Nigeria wawasili mbele ya bendera ya kundi la Boko Haram baada kuvunjwa kambi ya kijeshi ya kundi hilo katika jimbo la Yobe, mwezi Februari uliyopita.
Askari wa Nigeria wawasili mbele ya bendera ya kundi la Boko Haram baada kuvunjwa kambi ya kijeshi ya kundi hilo katika jimbo la Yobe, mwezi Februari uliyopita. AFP PHOTO/HO/NIGERIAN ARMY
Matangazo ya kibiashara

Mashambulizi hayo yalitokea huku kundi la Boko Haram likitoa mkanda mpya wa video na kudai kuwa kiongozi wao Abubakar Shekau bado ni mzima na anaedelea kuwaongoza.

Haya ndio mashambulizi mabya kuwahi kutokea katika jimbo hilo na hasa mjini Damaturu katika siku za hivi karibuni.

Shambulizi la kwanza lilitokea katika gala ndogo la chakula na kusabaisha vifo vya watu kadhaa, na lingine kutokea katika msikiti na lingine kutokea katika boma la mifugo nje ya mji huo.

Gavana wa jimbo hilo Ibrahim Gaidam ameshtumu mashambulizi hayo na kutaka serikali kuimarsiha usalama ili kukabiliana na Boko Haram.

Rais Muhamadu Buhari amelipa jeshi la nchi hiyo hadi mwezi Novemba kulitokomeza kabisa kundi hilo la Islamic State Afrika Magharibi.

Jimbo la Yobe, nchini Nigeria, linakabiliwa na masambulizi ya Boko Haram.
Jimbo la Yobe, nchini Nigeria, linakabiliwa na masambulizi ya Boko Haram. upload.wikimedia.org

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.