Wagombea wakuu katika uchaguzi wa urais warushiana cheche za maneno
Nchini Ufaransa, kuelekea duru ya pili ya uchaguzi wa urais siku ya Jumapili, wagombea wawili wakuu katika uchaguzi huo, rais Emmanuel Macron na Marine Le Pen, wanaendelea kunadi sera zao na kutafuta idadi kubwa wapiga kura watakaowachagua.
Imechapishwa:
Kuelekea mdahalo wa Televisheni hapo Jumatano wiki hii, wawili hao wameendelea kurushiana kauli za kisiasa kila mmoja akimkosoa mwenzake. Macron anatafuta muhula wa pili.
Le Pen ambaye anawania mara ya tatu, anasema anajiandaa kwenye mdahalo wa kesho.
Licha ya Macron kupewa nafasi kubwa ya kutetea kiti chake, wachambuzi wa siasa wanabashiri ushindani mkali siku ya Jumapili.
Marine Le Pen mgombea urais kupitia chama cha Rassemblement national na Emmanuel Macron, watamenyana katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais nchini Ufaransa, Aprili 24, 2022.