Pata taarifa kuu
UFARANSA-UCHAGUZI

Ufaransa: Wagombea urais warushiana cheche za maneno kuelekea duru ya pili ya uchaguzi

Nchini Ufaransa, wagombea wa urais, rais Emmanuel Macron na Marine Le Pen wameendelea na kampeni kuelekea duru ya pili ya uchaguzi wa urais Aprili 24.

Washindi wawili katika dura ya kwanza ya uchaguzi wa rais nchini Ufaransa mwaka wa 2022, Marine Le Pen na Emmanuel Macron ambao watachuana katika duru ya pili Aprili 24, 2022.
Washindi wawili katika dura ya kwanza ya uchaguzi wa rais nchini Ufaransa mwaka wa 2022, Marine Le Pen na Emmanuel Macron ambao watachuana katika duru ya pili Aprili 24, 2022. AFP - JULIEN DE ROSA,CHARLES PLATIAU
Matangazo ya kibiashara

Wagombea hao wawili wamerushiana maneno makali  baada ya maafisa wa usalama kumzuia, mwanamke aliyekuwa anaadamana kumshtumu Le Pen kwa kuwa karibu na rais wa Urusi Vladimir Putin baada ya kutoa sera yake ya kigeni iwapo atashinda uchaguzi.

Macron ambaye leo anaendelea na kampeni zake Magharibi mwa nchi, amemshtumu mpinzani wake kwa kuwa na mitizamo mikali aliyoiita ya kiimla.

Awali, Macron aliziita sera za Le Pen za ubaguzi wa rangi.

Naye, Le Pen amekataa kuomba radhi kuhusu misimamo yake hasa será ya mambo ya nje baada ya kukabiliwa na mwandamanaji.

Katika hatua nyingine, wagombea hao wawili wanajiandaa kumenyana katika mjadala wa televisheni wiki ijayo April 20 na kurushwa moja kwa moja kwenye Televisheni za TF1, France 2, Franceinfo miongoni mwa vyombo vingine vya Habari.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.