Pata taarifa kuu

Soka: Lionel Messi na Paris SG waachana rasmi

Paris Saint-Germain imerasimisha katika taarifa kwa vyombo vya habari Jumamosi kuhusu kuondoka mwishoni mwa msimu huu kwa mshambuliaji wake Lionel Messi baada ya miaka miwili akiichezea klabu hiyo katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris. Messi, 35, anacheza mechi yake ya mwisho na PSG Jumamosi jioni dhidi ya Clermont, katika siku ya mwisho ya Ligue 1. Mkataba wake utamalizika mwishoni mwa mwezi Juni.

Mwisho wa matukio ya Lionel Messi katika PSG.
Mwisho wa matukio ya Lionel Messi katika PSG. REUTERS - CHRISTIAN HARTMANN
Matangazo ya kibiashara

"Klabu ingependa kumshukuru kwa moyo mkunjufu mshindi huyo wa Ballon d'Or mara saba, mshindi chini ya rangi Nyekundu na Bluu za Kombe la Mabingwa na mataji mawili ya ubingwa wa Ufaransa," imeandika PSG katika taarifa kwa vyombo vya habari. "Asante kwa klabu hii, kwa jiji la Paris na kwa wakaazi wake kwa miaka hii miwili. Ninawatakia kila la kheri kwa siku zijazo, "amebainisha Mwargentina huyo katika taarifa ya PSG.

Kushindwa katika Ligi ya Mabingwa

Messi aliyewasili kwa shangwe kubwa mnamo 2021 kutoka klabu ya FC Barcelona, ​​​​amecheza mechi 74 na klabu ya Paris, akifunga mabao 32 na kutoa pasi nzuri 35. Lakini hatakuwa na uwezo wa kuiongoza PSG kuelekea lengo lake kuu, Ligi ya Mabingwa. "Paris Saint-Germain inajivunia kuwa na uwezo wa kuhesabu mchezaji bora katika historia yake katika safu na matakwa yake, kwa hisia fulani, mafanikio mengine mengi kwa Leo kwa maisha yake yote", imeandika klabu hiyo.

(Pamoja na AFP)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.