Droo ya hatua ya makundi kutangazwa Mei 24
Droo ya hatua ya makundi ya kutafuta ubingwa taji la klabu bingwa barani Afrika itatangazwa tarehe 24 mwezi Mei.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Vlabu vinane ambavyo vimefuzu katika hatua hii tayari vimefahamika na vitawekwa katika hatua ya makundi mawili, kila kundi na timu nne.
Kanuni za Shirikisho la soka barani Afrika CAF, linaweka wazi kuwa mechi hizo zitachezwa nyumbani na ugenini na mshindi atafuzu katika hatua ya nusu fainali.
Vlabu vilivyofuzu ni pamoja na:-
- ES Setif ya Algeria
- AS Vita Club ya DRC
- Al-Ahly ya Misri
- Zamalek ya Misri
- ASEC Mimosas ya Cote Dvoire
- Wydad Casablanca ya Morocco
- Enyimba ya Nigeria
- ZESCO United ya Zambia
Mabingwa watetezi wa taji hili msimu uliopita TP Mazembe waliondolewa baada ya kufungwa ugenini mabao 2 kwa 0 na sare ya bao 1 kwa 1 mjini Lubumbashi siku ya Jumatano.
Nayo droo ya hatua ya mwondoaano kuwania taji la Shirikisho itafanyika tarehe 21 mwezi Aprili.
Vlabu vilivyofuzu katika michuano hii ya Shirikisho vitakutana na vile vilivyoondolewa katika hatua ya taji la klabu bingwa barani Afrika.
Kutoka taji la Shirikisho
| Kutoka taji la klabu bingwa
|
Kutoka taji la Shirikisho
Sagrada Esperança
Misr El-Makasa
CF Mounana
Medeama
FUS Rabat
Kawkab Marrakech
Espérance de Tunis
Stade Gabèsie
Kutoka taji la klabu bingwa
MO Béjaïa
TP Mazembe
Al-Ahli Tripoli
Stade Malien
Mamelodi Sundowns
Al-Merrikh
Young Africans
Étoile du Sahel