Pata taarifa kuu
SUDANI KUSINI-SIASA

Rais wa Sudan na makamu wake wafikia makubaliano ya kuunda jeshi la pamoja

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na Makamu wake Riek Machar wamekubaliana kuunda jeshi la pamoja ikiwa ni hatua kubwa ya kutekeleza mkataba wa amani wa mwaka 2018. 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar (kushoto) na Rais Salva Kiir (kulia) wakiwa katika nyakati za furaha mjini Juba.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar (kushoto) na Rais Salva Kiir (kulia) wakiwa katika nyakati za furaha mjini Juba. ALEX MCBRIDE / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kiir na Machar, wamekubaliana kuunda jeshi la pamoja, moja ya masuala muhimu ambayo yamekuwa yakileta utata, na kusababisha kutotekelezwa kikakamilifu kwa mkataba huo wa amani uliolenga kuleta utulivu nchini humo. 

Martin Abucha, aliyesaini  makubaliano hayo kwa niaba ya upande wa upinzani wa Machar, amesema amani inahusu usalama na kwamba hii ni hatua waliyoipiga ya kufungua mwanya wa kuwa na serikali imara ya Sudan Kusini. 

Kwenye makubaliano hayo Upande wa rais Kiir utachukua asilimia 60 huku ule wa Machar ukichukua  asilimia 40 katika nyadhifa muhimu za uongozi wa jeshi, polisi na vikosi vingine vya usalama vya taifa. 

Hatua hii imekuja wiki moja baada ya kuwa na wasiwasi wa kutokea kwa mapigano kati ya vikosi vya rais Kiir na vile vya Machar na kuzua wasiwasi wa kuzuka kwa vita vingine kama ilivyokuwa kati ya mwaka 2013 hadi 2018. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.