Polisi yakabiliana na waandamanaji Sudan
Maandamano mapya dhidi ya kuongezeka kwa bei ya mkate yameongezeka jana Jumapili nchini Sudan huku polisi wa kuzuia ghasia wakisambazwa kwenye mji mkuu wa Khartoum kwa siku tano za maandamano ambayo tayari yamegharimu maisha ya takribani watu nane.
Imechapishwa:
Waandamanaji walichoma matairi na matawi ya miti mitaani na kujaribu kuharibu jengo la serikali kabla ya kuzuiwa na maafisa wa usalama, mashahidi alisema.
Viongozi wa upinzani nchini humo wanasema waandamanaji 22 wameuawa katika maandamani hayo yaliyoanza wiki iliyopita, kwa kupigwa risasi na polisi.
Polisi nchini Sudan wameendelea kukabiliana na waandamanaji katika miji mbalimbali.
Mamia ya waandamanaji jana, walikabiliana na polisi karibu na uwanja wa soka jijini Khartoum.