Pata taarifa kuu
UFARANSA-MISRI-USHIRIKIANO-ULINZI

Ufaransa kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na Misri

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean yves Ledrian amesema ufaransa iko tayari kuhakikisha ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi yake na Misri unaimarika zaidi katika mapambano dhidi ya ugaidi.

Vikosi vya usalama vya Misri karibu na kanisa la Mar Mina huko Helwan, kusini mwa Cairo, ambapo mashambulizi yaliua watu tisa tarehe 29 Desemba 2017.
Vikosi vya usalama vya Misri karibu na kanisa la Mar Mina huko Helwan, kusini mwa Cairo, ambapo mashambulizi yaliua watu tisa tarehe 29 Desemba 2017. REUTERS/Amr Abdallah Dalsh
Matangazo ya kibiashara

Ledrian aliyasema hayo punde baada ya kukutana na Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi jijini Cairo wakati wa ziara yake siku ya Jumapili, lakini pia kuzungumzia masuala ya biashara na hali ya Libya.

Mataifa haya mawili, yanaridhishwa na hali ya utulivu ambao umeanza kushuhudiwa nchini Libya kuelekea Uchaguzi Mkuu baadaye mwaka huu.

Ufaransa imeendelea kuunga mkono serikali ya Umoja nchini Libya na kupatikana kwa suluhu kuhusu mgogoro huo unaoendelea nchini humo.

Machafuko nchini Libya yaliyozuka baada ya kifo cha rais wa nchi hiyo Moamar Kaddafi, yamesababisha vifyo vya watu wengi na wengine wengi kulazimika kuyahama makazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.