Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-SIASA-AFRIKA

UNDP kuisadia Zimbabwe kuelekea maandalizi ya Uchaguzi Julai

Umoja wa mataifa umetangaza kuunga mkono uchaguzi mpya unaoandaliwa kufanyika mwezi Julai nchini Zimbabwe na kuitaka serikali ya taifa hilo kutoa kipaumbele cha dharura kwa uchumi wa taifa hilo.

Raisi wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa
Raisi wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa REUTERS/Denis Balibouse
Matangazo ya kibiashara

Achim Steiner, kiongozi wa mpango wa maendeleo katika umoja wa mataifa UNDP alikuwa ziarani jijini Harare na kukutana na raisi Emmerson Mnangagwa.

Steiner amesema Umoja wa mataifa unaendelea kuunga mkono mchakato wa maandalizi ya uchaguzi na jitihada za kuinua uchumi.

Uchaguzi wa uraisi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi August ambapo Mnangagwa atakabiliwa na ushindani tangu alipochukua madaraka kutoka kwa aliyekuwa kiongozi mkongwe wa taifa hilo Robert Mugabe, ambaye alijiuzulu mwezi Novemba baada ya kutawala kwa takribani miongo minne.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.