Mchungaji Evan Mawarire akamatwa Zimbabwe
Polisi nchini Zimbabwe wamemkamata Mhubiri maarufu Evan Mawarire ambaye pia ni mwanaharakati wa kisiasa baada ya mahubiri siku ya Jumapili.
Imechapishwa:
Polisi wanamshutumu kwa kuandika ujumbe wa uchichezi kupitia mitandao ya kijamii na kueleza kuwa serikali ya rais Robert Mugabe imeshindwa kuimarisha uchumi.
Mchungaji huyo amekuwa katika harakati za kumkosoa rais Mugabe na kuongoza maandamano kadhaa tangu mwaka 2016.
Mwezi Juni Mhubiri Evan Mawarire alifikishwa Mahakamani kujibu mashtaka ya uchochezi.
Wakati huo Bw Mawarire alifunguliwa mashtaka ya kushiriki katika mkutano usio halali na kusababisha usumbufu, madai ambayo aliyakanusha.
Mwezi Julai, alikamatwa kwa uchochezi na kuandaa maandamano dhidi ya rais Robert Mugabe na kesi yake inatarajiwa kusikilizwa mwezi Septemba.