Pata taarifa kuu
BURKINA-USALAMA-SIASA

Burkina Faso: makubaliano ya kutuliza ghasia yasainiwa kati ya majeshi

Nchini Burkina Faso, vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito na afisa wa wanajeshi wa kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP) wamesaini mkataba wa kutoshambuliana usiku wa Jumanne kuamkia Jumatano.

Katika Kasri la Mogho Naba, Mfalme wa jamii ya Mossi (katikati akivaa nguo za kiraia), wanajeshi wa vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mopito na afisa wa kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP) wakisaini makubaliano ya kutohasimiana Jumanne Septemba 22
Katika Kasri la Mogho Naba, Mfalme wa jamii ya Mossi (katikati akivaa nguo za kiraia), wanajeshi wa vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mopito na afisa wa kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP) wakisaini makubaliano ya kutohasimiana Jumanne Septemba 22 RFI/Olivier Rogez
Matangazo ya kibiashara

Wanajeshi wa kikosi cha ulinzi wa Raisa (RSP) wamekubali kurudi kambini na vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito kurudi nyuma kilomita 50 karibu na mji mkuu.

Hata hivyo wanajeshi wa kikosi cha ulinzi wa Rais hawakuweka chini silaha kama ilivyokua imeombwa na vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito. Mapema Jumanne jioni, jenerali Diendéré alihakikisha kuwa Michel Kafando ataachiliwa huru rasmi leo Jumatano.

Makubaliano hayo yamesainiwa Usiku wa Jumanne mjini Ouagadougou kati ya vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito na wanajeshi wa kikosi cha ulinzi wa Raiswaliofanya mapinduzi. Ni makubaliano ya kuepusha machafuko ambayo yanaeleza kwamba kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP) kinachoongozwa na jenerali Diendéré kitasalia kambini katika kambi yake wakati ambapo vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito vitarudi nyuma kilomita hamsini na mji mkuu.

Makubaliano hayo yamesaini rasmi mbele ya Mogho Naba, Mfalme wa jamii ya Mossi na kiongozi wa kiroho nchini Burkina Faso. Makubaliano hayo yalitiliwa saini na Korogho Abdulaziz, Kaimu mkuu wa kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP), na maafisa wanne waliotumwa na vikosi vya jeshi vinavyounga mkono serikali ya mpito. Baadhi ya viongozi wa wakuu wa vikosi vya jeshi vinavyouunga mkono serikali ya mpito ambao walianzisha jitihada ya kuelekea katika mji mkuu wa Burkina Faso, Ouagadougou ni wanafahamiana na wale wa kikosi cha ulinzi wa Rais (RSP).

Wakati huo huo ujumbe wa ECOWAS unaoundwa na marais kutoka jumuiya hiyo, unatarajia kuwasili mjini Ouagadougou ili kuendelea na mashauriano kati ya pande hizo mbili na kujadili kuhusu kumrejesha mamlakani Rais Michel Kafando na taasisi zingine za mpito.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.