UINGEREZA-EU-USHIRIKIANO-SIASA
Brexit: May aendelea kubanwa koo
Spika wa bunge nchini Uingereza John Bercow amesema hatakubali mapendekezo mengine kupigiwa kura kuhusu nchi hiyo kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya, iwapo Waziri Mkuu Theresa May hatawasilisha mswada mpya kwa wabunge.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Uamuzi huu unaendelea kumpa wakati mgumu Waziri Mkuu May, ambaye wiki iliyopita, mapendekezo yake yalikataliwa na wabunge wakati huu muda wa kujiondoa kwenye Umoja huo ukikarabia kufika.
Spika Bercow amesema mswada uliopingwa hauwezi kurudishwa bungeni bila ya kufanyiwa marekebisho.
Wabunge nchini Uingereza wanataka Umoja wa Ulaya kutoa muda zaidi, kuwezesha majadiliano ya mkataba utakaokubaliwa na kila mmoja.