Uchaguzi wa urais Urusi: Kampeni yenye hisia ya Vladimir Putin
Urusi ilifungua awamu ya mwisho ya kampeni za uchaguzi wa urais siku ya Jumamosi, Februari 17, uchagui ambao utafanyika kuanzia Machi 15 hadi 17 na ambao matokeo yake hayana shaka yoyote. Hii ni awamu ambapo televisheni inaweza kuandaa mijadala.
Imechapishwa:
Vladimir Putin, Kremlin tayari imetangaza, hatashiriki. "Ana shughuli nyingi," msemaji wake Dimitri Peskov alisema siku chache zilizopita. Kampeni yake inajitokeza kimsingi kwa sasa katika hali yenye hisia.
Mfano na maonyesho yenye kichwa "Urusi" ambayo yanafanyika huko Moscow. Lengo lake lililobainishwa ni kukuza urithi wa Kirusi na "mafanikio katika majimo", ikiwa ni pamoja na yale yaliyounganishwa kutoka Ukraine.