UINGEREZA-SIASA
Chama cha Boris Johnson chaangukia pua katika uchaguzi mdogo Shropshire Kaskazini
Nchini Uingereza, chama cha Conservative cha Waziri Mkuu Boris Johnson, kimepoteza kiti cha eneo la bunge la Shropshire Kaskazini katika uchaguzi mdogo ambao chama cha Liberal Democrats kimeshinda kwa Helen Morgan kuchaguliwa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Umuhimu wa eneo hilo hilo kwa chama cha Waziri Mkuu Johnson, ni kuwa kimekuwa kikishinda kwa karibu miaka 200. Johnson amesema anaelewa masikitiko ya wafausi wa chama chake.
Wachambuzi wa siasa wanasema matokeo haya mabaya ya chama cha Conservative, yanazua maswali kuhusu uimara wa uongozi wa Waziri Mkuu Boris Johnson.