Pata taarifa kuu
UJERUMANI-SIASA

Uchaguzi Ujerumani: Chama cha mrengo wa kati kushoto cha SPD chaibuka mshindi

Nchini Ujerumani, chama cha siasa za mrengo wa kati kushoto, SPD, kimepata ushindi mwembaba dhidi ya muungano wa kihafidhina wa CDU na CSU ambao umekuwa ukiongozwa na Kansela Angela Merkel anayemaliza muda wake.

Kulingana na matokeo rasmi ya awali, yaliyotolewa Jumatatu, Septemba 27, SPD inaongoza kwa pointi moja na nusu mbele ya muungano wa vyama vya kihafidhina vya CDU-CSU.
Kulingana na matokeo rasmi ya awali, yaliyotolewa Jumatatu, Septemba 27, SPD inaongoza kwa pointi moja na nusu mbele ya muungano wa vyama vya kihafidhina vya CDU-CSU. REUTERS - WOLFGANG RATTAY
Matangazo ya kibiashara

Matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika siku ya Jumapili, yanaonesha kuwa chama cha SPD kimepata ushindi mwembamba wa asilimia 25.7 na kukushinda chama  cha Kansela Merkel cha  CDU ambacho kimeibuka katika nafasi ya pili kwa asililia 24.1.

Chama cha SPD kinaongoza kwa asilimia mbili zaidi, wakati huu matokeo ya mwisho yanaposubiriwa.

Tayari kiongozi wa chama cha SPD Olaf Scholz amejitokeza na kusema matokeo yanaonesha kuwa, chama chake kimeshinda na kupewa nafasi ya kuongoza nchi hiyo ya bara Ulaya.

Naye Armin Laschet, kiongozi wa chama cha CDU licha ya kuwa nyuma, ana imani kuwa atafanikiwa kuunda serikali na kumrithi Kansela Merkel ambaye uongozi wake wa miaka 16 unafika mwisho. Hii ndio mara ya kwanza baada ya muda mrefu chama cha CDU kinapata matokeo mabaya.

Kufuatia vyama vya SDP na CDU/CSU, kuonesha nia ya kuunda serikali kutokana na uchaguzi huu wenye ushindani mkali, upande wowote unaweza kufanya hivyo, iwapo utapata washirika wanaohitajika kuunda serikali ya muungano.

Iwapo hali itakuwa hivyo, Kansela Merkel ataendelea kuongoza hadi pale serikali ya muungano itakapoundwa labda kufikia baadaye mwezi Desemba.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.