Mpango wa yuklia wa Iran: Washington na Tehran waendekea kutafautiana
Marekani na Iran zinaendelea kutofautiana kuhusu jinsi zinaweza kuanza tena kuheshimisha makubaliano ya nyuklia ya Iran ya mwaka 2015, licha ya maendeleo kadhaa yaliyopatikana katika mazungumzo ya hivi karibuni ya moja kwa moja huko Vienna, amesema afisa mwandamizi wa Marekani.
Imechapishwa:
Mazungumzo hayo yanatarajiwa kuchukua duru kadhaa, na matokeo yake bado hayajafahamika, afisa huyo mwandamizi kutoka wizara ya mambo ya nje amewaambia waandishi wa habari katika mkutano kwa njia ya simu.
Tofauti kuu zinahusu vikwazo ambavyo Marekani itahitaji kuondoa na kuhusu hatua ambazo Iran itahitaji kuchukua ili kukidhi majukumu ya kupunguza mpango wake wa nyuklia, afisa huyo amesema, huku akitaka jina lake lisitajwe.'
"Bado kuna tofauti, na wakati mwengine, tofauti kubwa, amesema. Hatuko karibu kuhitiisha mazungumzo haya. Matokeo bado hayajajulikana. Lakini kuna "hatua kubwa ambayo imepigwa", ameongeza."
Mazungumzo yataanza tena wiki ijayo.