MICHEZO-SOKA
Soka: Michuano ya klabu bingwa barani Afrika upande wa wanawake kuanza Septemba 5
Droo ya Makala ya kwanza, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika katika mchezo wa soka kwa upande wa wanawake, utakayofanyika jijini Cairo nchini Misri kati ya Novemba 5 hadi 19 imewekwa wazi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Kundi A linaundwa na timu za Wadi Delga ya Misri, AS Mande ya Mali, Malabo Kings ya Equitorial Guinea na Hasaacas Ladies kutoka Ghana.
Katika kundi B kuna Vihiga Queens kutoka nchini Kenya, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, AS Far ya Morocco na Rivers Angels ya Nigeria.
Mechi ya kwanza, itakuwa kati ya wenyeji Wadi Degla FC, ambao wameshinda taji la soka nchini Misri mara 12 dhidi ya AS Mande, ya Mali.