Pata taarifa kuu
ITALIA-EURO 2020

Rekodi ya michuano ya soka barani Ulaya

Italia ndio mabingwa wa soka barani Ulaya, baada ya kuishinda Uingereza mabao 3-2 kupitia mikwaju ya penalti, baada ya sare ya bao 1-1 katika mechi ya fainali iliyokwenda hadi katika muda wa ziada katika uwanja wa Wembley, jijini London.

Wachezaji wa Italia wakisherekea baada ya kushinda kombe la soka barani Ulaya, Julai 11  2021
Wachezaji wa Italia wakisherekea baada ya kushinda kombe la soka barani Ulaya, Julai 11 2021 Andy Rain POOL/AFP
Matangazo ya kibiashara

Uingereza ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 2 ya mchuano huo kupitia Luke Shaw, huku Leonardo Bonucci akisawazisha katika dakika ya 67.

Wachezaji wa Uingereza waliwaacha mashabiki wa nyumbani wakiwa wenye huzuni, baada ya Jadon Sancho, Bukayo Saka na  Marcus Rashford kukosa mikwaju ya penalti.

Mabao ya Italia yalitiwa kimyani na Federico Bernardeschi, Leonardo Bonucci na Domenico Berardi kuhakikisha kuwa kombe hilo linakwenda barani Ulaya.

Hii ni fainali ya kwanza, kufika katika hatua ya penalti tangu 1976 wakati Czechoslovakia ilipoishinda Ujerumani.

Hii ni mara ya pili kwa Italia kunyakua taji hili baada ya kufanya hivyo kwa mara ya kwanza mwaka 1968.

Mwaka 2000 na 2012 ilifika katika hatua ya fainali na kushindwa.

Orodha ya mabingwa wa zamani:-

Ujerumani-1972,1980, 1996

Uhispania-1964, 2008, 2012

Italia-1968, 2020

Ufaransa-1984, 2000

Jamhuri ya muungano wa Soviet-1960

Jamhuri ya Czech-1976

Ureno-2016

Uholanzi-1988

Denmark-1992

Ugiriki-2004

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.