Mechi za robo fainali kuwania taji la vijana wasiozidi miaka 20 kunguruma
Mechi za robo fainali kuwania taji la soka kwa vijana wasiozidi miaka 20 inaanza kuchezwa siku ya Alhamisi nchini Mauritania.
Imechapishwa:
Mechi ya kwanza, itakuwa gani ya Cameroon na Ghana, mchuano unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, katika uwanja wa Olympique jijini Nouakchott.
Ghana wanaocheza katika mashindano haya mara ya 12, wanatafuta taji la nne, tangu waliposhinda mara ya mwisho mwaka 2009.
Cameroon, nao wanaoshiriki kwenye michuano ya 10 wanasaka taji lake la pili kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 26.
Morocco nayo itachuana na Tunisia katika mechi nyingine.
Mechi ya robo fainali, Februari 26 2021:-
Burkina Faso vs Uganda
Jamhuri ya Afrika ya Kati vs Gambia
Fainali itachezwa tarehe 6 mwezi Machi mwaka 2021.