GHANA-UHOLANZI-SOKA
Ghana yafufungwa Uholanzi 4-0
Timu ya taifa ya soka ya Ghana ya wasichana wasiozidi miaka 20, wamefungwa katika mechi yake ya pili mfululizo katika fainali ya kombe la dunia inayoendelea nchini Ufaransa.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ghana ilifungwa na Uholanzi mabao 4-0. Mechi ya kwanza Black Princesses walianza vibaya baada ya kufungwa na Ufaransa mabao 4-1.
Mechi yake ya mwisho itakuwa dhidi ya New Zealand siku ya Jumapili, kabla ya kuyaaga mashindano hayo.
Wawakilishi wengine wa Afrika, Nigeria wanacheza na Haiti leo Alhamisi baada ya kuanza vibaya kwa kufungwa na Ujerumani 1-0.