Pata taarifa kuu
SOKA-UEFA-BARCELONA-BAYERN MUNICH

Bayern na Barcelona zajitupa uwanjani

Michuano ya nusu fainali za Kombe la Mabingwa barani Ulaya katika mechi ya marudiano inatazamiwa kuchezwa Jumanne jioni wiki hii, kati ya Barcelona ya Uhispania na Bayern Munich ya Ujerumani.

Mchezaji wa Morocco, Mehdi Benatia (kulia)akiichezea Bayern Munich wakati ilipofungwa na Barcelona mabao 3-0 katika michuano ya nusu fainali za Kombe la Mabingwa barani Ulaya katika mechi ya marudiano.
Mchezaji wa Morocco, Mehdi Benatia (kulia)akiichezea Bayern Munich wakati ilipofungwa na Barcelona mabao 3-0 katika michuano ya nusu fainali za Kombe la Mabingwa barani Ulaya katika mechi ya marudiano. Reuters / Kai Pfaffenbach
Matangazo ya kibiashara

Bayern  Munich  leo  Jumanne jioni inajaribu  kubadilisha  matokeo ya mabao  3-0 kipigo ilichopata  wiki  iliyopita  dhidi  ya Barcelona  katika  mchezo  wa kwanza  wa  nusu  fainali  ya  za Kombe la Mabingwa barani Ulaya.

Bayern  ambayo  itawakosa wachezaji wake muhimu katika mchezo huo kutokana na kukumbwa  na  matatizo  makubwa  ya   majeruhi  katika kikosi  chake  itakuwa  katika  uwanja  wake  wa  Allianz  Arena  ikiikaribisha Barcelona usiku  wa  leo.

Katika mechi ya awali, mabao mawili ya Barcelona yaliwekwa wavuni na Lionel Messi. Bao la kwanza liliingizwa katika dakika ya 76, huku bao la pili liwekwa wavuni katika dakika ya 80.

Bao la tatu lilifungwa na Neymar katika dakika 1 za nyongeza baada ya dakika 90 za mchezo.

Katika mechi ya awali Barcelona ilionekana kutawala mpira katika kipindi cha pili hasa pale Messi alipoifungulia klabu yake bao la kwanza.

Katika kipindi cha kwanza klabu zote mbili zilikua sare, na zilionekana zikicheza vizuri na zikiwa na nguvu sawa.

Hadi kipenga cha mwisho Bayern Munich imejikuta ikiangukia pua.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.